Msanii wa Muziki wa Bongio Fleva, Barakah the Prince amesisitiza kuhusiana na kumchukia msanii mwenzake Alikiba tena siyo kumchukia tu bali hampendi.
Akizungumza na chombo kimoja cha habari nchini, Barakah the Prince amesema kuwa;
"Ni kweli bado namchukia sana Alikiba na hilo haliwezi kujificha mpaka leo. Kwa sababu kuna vitu personal vinavyofanya nimchukie Kiba. Mimi sio lazima nimpende Alikiba" amesema Baraka The Prince.
Ikumbukwe tu si mara ya kwanza msanii huyo kuweka wazi kuhusiana na kumchukia Kiba, ila awali alishawahi kuzungumza hivyo kwenye Media lakini hakuweza kuweka sababu zipi zilizomfanya amchukie kiasi hicho."