Mbunge wa Morogoro Kusini Mashariki, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ amesema kwenye muziki hawapendi machawa.
Tale ameyasema hayo alipokuwa amepewa chalange ya picha katika kipindi cha Big Sunday ambapo alipowekewa picha ya Chawa na Kiki yeye akasema anachagua kiki.
“Nachagua kiki. Sipendi kabisa machawa. I hate chawa. Unajua hawa wanafanya sometime wanaharibu hata kazi ya msanii ambaye amewekeza pesa nyingi,” alisema Babu Tale.
Hata hivyo, lebo ya Wasani inatajwa kumiliki machawa wengi akiwemo Baba Levo ambaye kuna wakati aliwahi kumchana hadharani na Baba Levo alipojaribu kujibu, inasemekana kuwa alisimamishwa kazi kisha baadaye akarudishwa.