Mathew Knowles, Baba mzazi wa mwanamuziki nyota wa muziki wa pop duniani, Beyoncé, amekuja juu baada ya jina la binti yake kutokuwepo kwenye list ya wasanii watakaowania Tuzo za Muziki wa Country za mwaka huu.
Majina ya watakaowania tuzo hizo yalitangazwa hivi majuzi, huku jina la Beyoncé likikosekana licha ya kuwa na wimbo nambari moja wa muziki wa 'Country' pamoja na albam iliyotoka mwezi March mwaka huu.
Mzee Mathew Knowles aliwashutumu waandaaji wa tuzo hizo akiwaita wabaguzi wa rangi kwa kuwa hawaangalii uwezo na mafanikio ya mtu bali rangi.
Albamu ya Beyoncé ‘Cowboy Carter’ ndiyo albamu mpya ya 'Country' iliyopewa sifa kedekede na ambayo imeuza zaidi mwaka huu.