Menu ›
Burudani
Fri, 18 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mtangazaji wa Wasafi FM, Baba Levo ameweka wazi sababu iliyomfanya Harmonize akatae kualikwa kwenye Wasafi Festival na kisha baadaye kukubali kuwa yupo tayari kushiriki.
Baba Levo amesema, awali Harmonize alikataa kushiriki akijua kwa kufanya hivyo shoo hiyo inayotarajiwa kufanyaka nyumbani kwao Mtwara lakini alipoona 'wakubwa' kibao wamekubali ndipo naye akajirudi.
"Yule alidhani akisema hatakuwepo sisi hatutapata watu sasa alipoona wasanii wakubwa karibu wote wamesema watakuwepo ndipo akaanza kujirudi," alisema Baba Levo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live