Menu ›
Burudani
Mon, 12 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baba Levo amefanya mazungumzo na Ayo Tv ambapo amefunguka sababu za kuzuka kwa ugomvi kati yake na Harmonize usiku wa jana.
Baba Levo anadai kuwa kuna tajiri alishinda pesa zaidi ya Bilioni 1 wakiwa Casino, baada ya kushinda tajiri alimpatia Baba Levo Milioni 10 ili agawane na wengine waliopo hapo Casino akiwemo Harmonize.
Kwa mujibu wa Baba Levo anadai kuwa Harmonize alimpora Milioni 5 jambo ambalo kwa upande wake hakuridhia.
Katika harakati za kumtaka Harmonize atoe pesa hizo ndipo Harmonize alimkunja shingoni na kuanza kufanya vurugu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live