Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Baba Diamond ashiriki hafla ya mjukuu wake

86038 Pic+mond Baba Diamond ashiriki hafla ya mjukuu wake

Thu, 28 Nov 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Abdul Juma ambaye ni baba mzazi wa msanii wa Tanzania, Diamond Platnumz ni kati ya watu walioshiriki hafla ya mjukuu wake iliyofanyika leo Jumanne Novemba 26, 2019.

Mtoto huyo wa Diamond na  Tanasha Donna alizaliwa Oktoba 2, 2019 jijini Dar es Salaam na kupewa jina la Naseeb Junior kwa kuwa alizaliwa siku na mwezi aliozaliwa Diamond ambaye jina lake halisi ni Naseeb Abdul.

Baba yake Diamond aliwasili nyumbani kwa mwanaye saa 8:45 mchana muda mfupi baada ya kuanza hafla hiyo.

Baadhi ya wasanii waliohudhuria hafla hiyo ni  Queen Darleen, Rayavany, Romy Jones, Laizer, Moze Iyobo na Kulwa Kikumba maarufu  Dude.

Chanzo: mwananchi.co.tz