IKIWA ni saa kadhaa baada ya kusambaa kwa taarifa kutoka nchini Kenya zikidai kuwa mke wa supastaa wa Bongo Fleva, Alalikiba aitwaye Amina ametaka talaka akidai kuwa mumewe huyo hatimizi majukumu yake kama mume/ baba katika familia, Kiba ameibuka na hili jipya.
kupitia ukurasa wake wa Instagram, ikiwa leo kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa mtoto wake, Keyaan, Kiba amempost na kuandika; "Halizuki jambo bila Mwenyezi Mungu kutaka yote kheri, happy birthday son nakupenda sana usinisahau @keyaanalikiba #kingkiba''
Imeelezwa kuwa, mke wa Kiba amekwenda katika mahakama ya kadhi akitaka apewe talaka na muewe huku pia akiiomba mahakama hiyo iamwamuru Kiba kutoa Tsh milioni 4 kila mwezi kwa ajili ya matumizi ya watoto wake wawili aliozaa na mwanamke huyo.