Msanii kutoka nchini Nigeria Ayra Starr yupo tayari kuja kutumbuiza kwenye jukwaa moja na Mfalme wa Bongo Flava Alikiba kwenye tamasha la Lockin255 linalotarajiwa kufanyika Jumamosi ya Mei 20, mwaka huu pale Super Dome Masaki jijini Dar es Salaam.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ayra Starr kwenye Instastory ameweka cover ya show hiyo na kuandika "Tanzania Soon".
Kumbuka hili ni tamasha linaloenda kuwakutanisha Alikiba na Ayrastarr kwenye jukwaa moja kila mtu anatamani kuiona siku hii ya kihistoria.
Milango ya Super Dome pale itaachwa wazi kuanzia saa 12:00 jioni na tiketi zote zinapatikana kwenye App ya Nilipetz.