Aunty Ezekiel Grayson Jujuman; ni supastaa wa Bongo Movies ambaye anasema kuwa, amekuwa akipata dili za kutosha ambazo zinamuwezesha kuendesha maisha yake bila hata ya kuwa na meneja kama ambavyo wanafanya mastaa wengi Bongo.
Aunty ambaye ni mama wa watoto wawili, anasema kuwa, kutokana na hilo, kwake bado hajaona ulazima wa kuwa na meneja katika kazi zake za sanaa na mambo mengine ya ubalozi.
“Kwa upande wangu napata dili za kutosha maisha yanakwenda kwa hiyo sidhani kama kuna tofauti ya kuwa na meneja na kutokuwa na meneja na kwa sababu pengine sijawahi kuwa chini ya menejimenti,” anasema Aunty.