Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aunt Ezekiel ‘amfumbia macho’ ex Girl Friend wa Mose Iyobo

5277 22278202 2380124632212768 3308110491439595520 N TZW

Sun, 25 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa Filamu Bongo, Aunt Ezekiel ambaye pia ni mpenzi wa Mose Iyobo amesema alikuja kugundua kugombana na mpenzi wa zamani wa Iyobo ‘Mwengi’ ni kitu ambacho hakina maana yoyote.



Muigizaji huyo amesema hata wangeendelea kugombana kusingebadilisha majina ya watoto wao ambao wamezaa na Iyobo na si kitu kizuri kwa watoto hapo baadae.

“Katika vitu ambavyo vilipita nilishaandika nikasema sitakaa nigombane na Mwengi tena kwa sababu nimekuja kugundua ni ujinga mwisho wa siku hata nigombane naye miaka mia yule mtoto wake hawezi kuja kubadilika jina,” amesema na kuongeza.

“Lazima mwisho wa siku ataitwa fulani fulani Iyobo, hivyo hivyo kwa Cookie, kwa hiyo wale tayari ni ndugu halafu sasa hivi mitandao ni mengi baadae wakija kuone mama yangu na huyu walikuwa wanagombana itakuja kuwaletea shida watoto,” Aunt Ezekiel ameiambia Bongo5.

Kwa sasa Aunt Ezekiel yupo mbioni kuachia filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la Mama, katika filamu hii amecheza na mwanae, Cookie.

Chanzo: bongo5.com