Mwanamke mmoja huko nchini Uingereza aliyefahamika kwa jina la Jennifer Tait amekutana na hukumu ya kwenda jela miaka miwili baada ya kuwalaghai wanaume 3 kuwa ana ujauzito wao.
Mwanamke mmoja huko nchini Uingereza aliyefahamika kwa jina la Jennifer Tait amekutana na hukumu ya kwenda jela miaka miwili baada ya kuwalaghai wanaume 3 kuwa ana ujauzito wao. Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 37 alikutana na wanaume hao kwenye mtandao wa Tinder na inadaiwa aliwapeleka wanaume hao Hospital kwa muda tofauti na kutengeneza vyeti feki kuwa ni mjamzito kitu ambacho mahakama ilibaini kuwa ni uongo na alikuwa na njama zake.