Menu ›
Burudani
Thu, 14 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanaume mmoja nchini Kenya anayefahamika kwa jina la Henry Ochola Midiwo anashtakiwa kwa kushindwa kulipa bili ya Ksh 7000 sawa na Tsh 140,838 kwa kuagiza chakula na pombe kali hotelini akiwa na mpenzi wake.
Henry ameachiwa kwa dhamana ya Ksh 200,000 na kesi yake inatarajiwa kusikilizwa April 25 mwaka huu.
Taarifa zinasema kuwa, siku ya tukio Henry alifika hotelini akiwa na mwanamke anaedhaniwa kuwa ni mpenzi wake, ambaye aliagiza chakula na pombe kali kisha wakaelekea chumbani pamoja. Baada ya masaa kadhaa alipelekewa bili yake na hakuwa na uwezo wa kuilipa.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live