Kampuni ya Apple imesogeza mbele mradi wake (Project Titan) wa kutengeneza magari yasiyo na usukani wala pedeli hadi mwaka 2026. Hii ni kutokana na uhaba wa teknolojia lakini pia kutikisika kwa uongozi wa timu ya wahandisi.
Kampuni ya Apple imesogeza mbele mradi wake (Project Titan) wa kutengeneza magari yasiyo na usukani wala pedeli hadi mwaka 2026. Hii ni kutokana na uhaba wa teknolojia lakini pia kutikisika kwa uongozi wa timu ya wahandisi. Tangu mwaka 2014, kampuni hiyo iliweka wazi kuja na mradi huo ambao magari yatakuwa yakijiendesha kiteknolojoa ‘Automatic’ pasina dereva kutumia usukani wala kukanyaga pedeli chini. Kwa mujibu wa taarifa, magari hayo ya Apple yataingia sokoni kwa bei ya ($100,000) zaidi ya TSh. Milioni 233.