Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Angel Nyigu, Dansa aliyefanya balaa ndani ya Jeje,Cheche

Nyigu+pic Angel Nyigu, Dansa aliyefanya balaa ndani ya Jeje,Cheche

Sat, 17 Oct 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Ni kama wazazi walijua hapo baadaye atakuja kuwa nani.Hii ni baada ya kumpa jina la Angle Batolomeo Nyigu.

Jina ambalo limemuwezesha pia kupata jina la kisanii la ‘Angel Nyigu’ likihusishwa na sanaa anyoifanya ya kudansi ambapo ndani yake kuna ukataji mauno.

Angel Nyigu, ni mmoja ya madansa wa kike walio na maarufu katika lebo ya WCB kwa sasa na hii ni kutokana na kuonekana kwenye video nyingi za wasanii waliopo kwenye lebo hiyo ikiwemo Cheche, Jeje na nyingine nyingi.

Akielezea safari yake hadi kujikuta anakuwa dansa maarufu, Angel anasema ilianzia katika mshindano ya kusaka vipaji ya Kinondoni Search yaliyofanyika mwaka 2015, ambayo yaliandaliwa na Paul Makonda, wakati huo akiwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni.

“Katika mashindano hayo yaliyofanyika Machi 2015 nikiwa kidato cha nne niliweza kuwa msichana pekee niliyeingia fainali kwa upande wa kudansi na hapo ndipo milango ilipoanza kufunguka kwa kufanya kazi na watu na makundi mbalimbali ya kudansi na tasnia ya muziki,”anasema.

Wakati kuhusu kuwa familia ya WCB, anasema ni baada ya kufanya kazi na Queen Darleen ambaye aliku akihitaji dansa kwa ajili show iliyofanyika Mtwara na hapo ndio ikawa mwanzo wa kuwa dansa wake na ndipo uongozi ulipomuona na kumuita kufanya kazi na wasanii mbalimbali wa lebo hiyo.Ukiachilia mbali Queen Darleen, pia alishafanya kazi na Rosa Ree na Vanessa Mdee na Pam D.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz