Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Amlazimisha mpiga picha wake amtazame akifanya mapenzi

Megan Kesi Amlazimisha mpiga picha wake amtazame akifanya mapenzi

Wed, 24 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mpiga picha wa rapa kutoka nchini Marekani, Megan Thee stallion anayejulikana kwa jina la Emilio Garcia amemfungulia mashtaka rapa huyo maarufu Duniani kwa kosa la kumlazimisha kumtazama akiwa anafanya mapenzi na mtu mwingine kwenye gari.

Mpiga picha huyo alianza kufanya kazi na Megan mwaka 2018 kabla ya mwaka uliofata yaani 2019 kumuajiri kama mpiga picha wake rasmi.

Emilio katika mashtaka aliyomfungulia Megan katika mahakama ya Los Angeles nchini Marekani amesema walisafiri pamoja June mwaka 2022 kwenda nchini Uhispania kikazi na ndipo majira ya usiku boss wake huyo alimuita kwenye gari alikokuwa yupo na mtu mwingine wakifanya mapenzi na kumwambia Emilio atazame tukio hilo.

Mpiga picha huyo amesema baada ya tukio hilo siku moja baadae Megan alimuita na kumwambia anapaswa kufunga mdomo wake na asizungumze hilo popote.

Emilio amesema tukio hilo lilimfanya ajisikie vibaya kiasi cha kutamani kuacha kazi wazo alilolifanyia kazi mwaka 2023 alipofanya maamuzi ya kuacha kazi rasmi.

Mwanasheria wa Emilio amefunguka kuwa kitendo hicho alichofanyiwa mteja wake si sawa na ni kinyume na sheria za kazi .

Kwa upande wa mwanasheria wa Rapa Megan amekana shitaka hilo akisema ni la uongo na limetengenezwa ili watu wajipatie fedha .

Chanzo: www.tanzaniaweb.live