Menu ›
Burudani
Mon, 20 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
‘Rapa’ kutoka nchini Marekani, AmberRose anadai kuwa anamchukulia Wiz Khalifa kama mpenzi wake wa maisha kwa sababu kuachana kwao kulimfanya alie kwa miaka mitatu.
Msanii huyo akiwa katika mahojiano na Podcast ya No Jumper ameeleza amekua akijilaumu kuachana na Wiz, hivyo mpaka sasa atabaki kuwa mpenzi wa maisha yake yote ingawa wametengana.
Amber ambaye ana mtoto mmoja na Wiz Khalifa, aliendelea kwa kusema ukaribu ambao wanao kwa sasa kwenye malezi ya mtoto wao pia unatokana na upendo wao wa zamani, wawili hao waliachana mwaka 2014.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live