Menu ›
Burudani
Tue, 22 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Swali linalifikirisha huko mitandaoni ni kwamba, Afisa Habari wa Yanga, Ally Kamwe na mwanamitindo Hamisa Mobetto ni wapenzi? Hii ni kutokana na namna wanavyopeana jumbe za hapa na pale mitandaoni.
Ujumbe mpya, Kamwe amemfikishia amemuambia Mobetto kuwa amesikia alivyomuita ‘kid’ na kudai kuwa siku akilewa atatoka hadharani na kumjibu mwanadada huyo kama yeye ni mtoto au mkubwa.
Kamwe amezungumza hayo baada ya kuulizwa nini kinaendelea kati yake na Hamisa. Wawili hao wamekuwa wakipeana jumbe tata mara kwa mara na wachambuzi wa mambo kuhisi kwamba kuna jambo linaendelea kati yao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live