Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Aliyemuua ndugu yake Rihanna afikishwa Mahakamani

1147 Rihana 603x400 TZW

Fri, 5 Jan 2018 Chanzo: millardayo.com

Leo January 5, 2918 Mwanaume mmoja amekamatwa na kufunguliwa mashtaka ya mauaji ya Tavon Kaiseen Alleyne, 21 ambaye ni ndugu wa mwanamuziki wa kimataifa Rihanna.

Taarifa zilizotolewa na Nation News zimesema, “kijana huyo anafahamika kama Shawayne Dashawn Williams ana umri wa miaka 23, amefunguliwa mashtaka ya mauaji hayo ya Alleyne ambayo yametokea wiki iliyopita katika sikukuu ya Christmas.”

Shawayne amefikishwa Mahakamani kwa mara ya kwanza na kesi hiyo imeahirishwa na mtuhumiwa amerudishwa gerezani huku hukumu ya kesi hiyo ikipangwa kutolewa January 31, 2018.

Kabla ya tukio marehemu Alleyne alikuwa akitembea karibu na nyumba yake majira ya saa 1 usiku kabla ya kufatwa na mtu asiyefahamika na kisha kupigwa risasi. Hata hivyo Alleyne alikimbizwa hospitali ya Queen Elizabeth iliyopo Bridgetown lakini alifariki dunia.

Wakati huo huo marehemu Tavon Alleyne alikuwa na Rihanna saa moja kabla ya kufariki dunia wakisherehekea pamoja sikukuu ya Christmas.

MSIBA: MWANAMUZIKI MKONGWE WA DANSI AFARIKI DUNIA

FULLVIDEO: BABU SEYA NA PAPII KOCHA RASMI WAINGIA STUDIO, WAZUNGUMZA HAYA

Chanzo: millardayo.com