Chawa Pro Max, Baba Levo amecharuka kuwa, yeyote ambaye amehusika kumdhulumu Diamond shilingi Bil. 4 alizotaka kununua ndege ni mpuuzi.
Baba Levo ametoa kauli hiyo wikiendi iliyopita akiwa mkoani Shinyanga wilaya ya Kahama, alipokwenda kufanya shoo ya Wasafi Festival.
"Kuna majamaa ya hapa Bongo hayo tunayalaani kwa kuhusika kwao kutaka kumdhulumu Diamond lakini wale wa nje pia waliohusika ni wapuuzi tu. Yeyote aliyehusika ni mpuuzi tu, kama wanafikiri wamemkomoa Diamond ndio kwanza anaendelea na mishe zake. "Ametapeliwa Bil 4 lakini hajayumba. Na niwahakikishie lazima tutadili nao tu mpaka kieleweke," alisema Baba Levo.