Menu ›
Burudani
Wed, 3 Jun 2020
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa wa muziki ndani na nje ya Tanzania Alikiba, ametimiza ahadi yake aliyowaahidi mashabiki wake ya kwamba, ataachia kazi mpya mara baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kuisha.
Hilo limejidhirisha kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram, baada ya kutangaza kuachia kazi mpya iitwayo "so hot".
"Tuna makubaliano mazuri kwenye uongozi na mimi ndiyo C.E.O, lazima watu wawe na muamko mzuri kwa sababu watu wamenimiss, nawaambia mashabiki zangu kwamba mwezi wa Ramadhan ukiisha, kuna ngoma ya ajabu sana inakuja, nawaambia ukweli maana sijawahi kusema hivi" amesema Alikiba.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live