Kuelekea shoo ya Harmo Night iliyofanyika juzi Desemba 25, 2022, Msanii Harmonize alotoa ahadi ya kwamba ndio siku atakayo mtambulisha meneja wake mpya
Harmonize alitumia Insta Story kutoa taarifa hiyo kwa mashabiki na watu wote wanao mfuatilia.
Harmonize aliendelea mbele zaidi na kumpa sifa Meneja wake mpya huyo kwa kununua ticket ili kuhudhuria shoo hiyo.
Mpaka sasa haijulikani Meneja mpya ni yupi kwa maana hakutambulishwa mtu yeyote kwenye ile shoo.
Swali ni Je, Meneja aliumwa kama Diamond?
Hii sio mara ya kwanza kwa Harmonize ku ahidi mambo na kuto yatimiza. Utakumbuka mambo kama Konde Fm, Konde Cigarette na nyinge.