Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Adidas yafanikiwa kujiondoa kwenye mkataba na rapa Kanye West

Adidas Yafanikiwa Kujiondoa Kwenye Mkataba Na Rapa Kanye West Adidas yafanikiwa kujiondoa kwenye mkataba na rapa Kanye West

Wed, 17 Apr 2024 Chanzo: Bbc

Kampuni ya Adidas hatimaye imejinasua kutoka kwa mgogoro mkali wa kisheria na rapa Kanye West na inasema inatarajia kupata faida ya euro milioni 700 mwaka 2024.

Mwezi Februari kampuni hiyo kubwa ya mavazi ya Ujerumani ilisema inapanga kuuza bidhaa zake za Yeezy zilizosalia kutokana ushirikiano wake na West kwa bei nzuri.

Tamko la kusisimua lililotolewa Jumanne na Adidas linakuja mwezi mmoja baada ya kampuni kupata hasara kwa mara ya kwanza katika kipindi cha miaka 30.

Inatengeneza viatu vya Samba, Gazelle na Campus. Kampuni hiyo ilisema kuwa takwimu zilizorekebishwa zilikuwa euro milioni 200 zaidi ya ilivyotabiriwa hapo awali na kushuka hadi kiwango bora kuliko ilivyotarajiwa robo ya kwanza ya mwaka.

Kampuni hiyo ilisema faida yake ya robo mwaka ilifikia euro milioni 336, kutoka euro milioni 60 mwaka mmoja kabla ya kukumbwa na mvutano na West.

Adidas zaidi ilisema kuwa imeuza bidhaa nyingine za Yeezy zenye thamani ya euro milioni 150 katika robo ya mwaka, kwa faida ya karibu euro milioni 50.

Chanzo: Bbc