Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Adele atamani Mtoto wa kike

Adele Marekani Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Adele

Tue, 21 May 2024 Chanzo: Mwanaspoti

Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Adele ameweka wazi kuwa kwa sasa yupo tayari kuanzisha familia na mpenzi wake Rich Paul, na endapo atabahatika kupata mtoto basi anatamani awe wakike.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram Adele ameeleza kuwa atakapomaliza majukumu yote ya show anatamani kuwa na mtoto wa kike kutokana sasa tayari anaye wa kiume aitwaye Angelo (11) aliyempata na mpenzi wake wa zamani Simon Konecki.

Uhusiano wa Adele na Paul ulianza mwanzoni mwa 2021, huku mwishoni mwa mwaka 2023 Adele alithibitisha kufunga ndoa na Rich kwenye tamasha la vichekesho la rafiki yake Alan Carr.

Chanzo: Mwanaspoti