Mpigapicha na mfanyabiashara, Abu Salami amedai kuwa msanii kutoka nchini Nigeria Davido hana pesa bali msanii huyo anaishi maisha ya uongo.
Hii inakuja baada ya mpigapicha huyo kutoelewana na Davido katika simu kuhusiana na deni la N218 Milion kwa ajili ya mradi wa watoto ambapo amedai kuwa msanii Burna Boy na Rema ni matajiri kushinda Davido.
Hii ni mara ya pili mwaka huu kwa Davido kushutumiwa kwa kushindwa kutimiza majukumu ya kimkataba, hapo awali, Rais wa zamani wa Shirikisho la ‘Soka’ la Nigeria, Amaju Pinnick, alimuita hadharani Davido kwa kutoheshimu mkataba wake nao.
Davido ambaye kwasasa anatamba na album yake ya ‘Timeless’ huku wimbo ambao umeibeba albamu hiyo ukiwa ni ‘Unavailable’.