Msanii wa muziki Abigail Chamangwana 'Abby Chams' amemjibu shabiki aliyeuliza kwanini anamchukia Paula Kajala na amesema kuwa hawezi kumchukia mtu ambaye hajui kazi anayofanya.
Ikumbukwe kuwa, Abby Chams aliingia kwenye ugomvi na paula pamoja na mama yake Kajala kwa kile kilichodaiwa kuwa waliikataa ngoma ambayo Abby alifanya na Marioo ambaye ni mpenzi wake na Paula.
"Mimi siwezi kumchukia mtu mwanamke mwenzangu siwezi kumchukia mtu yeyote ambaye ameumbwa na Mungu lakini nimejibu tu hili swali kwa sababu nimewaahidi nitajibu maswali yote.
"Lakini ningependa mniulize kuhusu kazi yangu kwasababu mimi sioni umuhimu kuongelea watu ambao hata hatujui kazi zao ni nini ila tu ku-trend kwa sababu ya kudate wanaume," amesema Abby Chams.