Menu ›
Burudani
Wed, 6 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa mkongwe wa Hip Hop nchini Marekani Ja Rule hivi karibuni amefanya mahojiano na Mtangazaji Piers Morgan (Uncensored) na kushea stori yake kuwa aliwahi kumpiga vibaya hasimu wake Rapa #50Cent katika moja ya pambano la ngumi miaka ya nyuma.
"Mbona imeshatokea tayari, nilimpiga vibaya mno, mimi ndio nilishinda, jaribu kufuatilia, wewe fuatilia watakwambia," amesema Ja Rule katika interview hiyo.
Inadaiwa wawili hao kutokea jiji la New York wamekuwa na tofauti kwa kipindi kirefu sasa, wamekuwa na ‘beef’ kwa miaka 25.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live