Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

50 Cent amdhihaki Madonna

Madonna50cent 50 Cent amdhihaki Madonna

Sun, 29 Oct 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

‘Rapa’ mkongwe kutoka nchini Marekani, #50Cent inadaiwa kuwa ameudhihaki muonekano wa mwanamuziki #Madonna kwa kumcheka baada ya ‘kumposti’ katika ukurasa wake wa Instagram.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari inaelezwa kuwa ‘rapa’ huyo aliingia kwenye mtandao wake wa #Instagram na kuweka picha ya Madonna akiwa amevalia vazi la dhahabu akimfananisha na mdudu mweusi.

Hata hivyo Madonna mpaka sasa hajatoa maoni yoyote kuhusiana na dhihaka hiyo aliyoifanya 50 Cent kwa kitendo cha ‘kupost’ picha yake na kumfananisha na mdudu.

Imekuwa kawaida kwa ‘rapa’ huyo kumkashifu mwanamuziki huyo maarufu wa nyimbo za Pop, mwaka 2022, 50 Cent alifanya hivyo hivyo kwa ‘kuposti’ mitandaoni picha mbaya ya Madonna.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live