Dar es Salaam. Waziri wa Maji nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa leo Alhamisi Desemba 19, 2019 amefika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutoa ushahidi katika kesi ya jinai namba 3/2017 inayomkabili Winfrida Masawe.
Dar es Salaam. Waziri wa Maji nchini Tanzania, Profesa Makame Mbarawa leo Alhamisi Desemba 19, 2019 amefika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kutoa ushahidi katika kesi ya jinai namba 3/2017 inayomkabili Winfrida Masawe. Masawe wanakabiliwa na mashtaka manne ikiwemo ya kujipatia Sh700,000 kwa njia ya udanganyifu akijifanya yeye ni waziri huyo. Alitenda kosa hilo wakati Profesa Mbarawa alipokuwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.