Tue, 12 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mahakama imemaliza kusoma muhtasari wa ushahidi wa upande wa mashtaka na utetezi wa washtakiwa katika kesi ya mjane wa bilionea Msuya na mwenzake, ambapo wazee wa baraza wameomba ahirisho la muda kabla ya kutoa maoni yao kuishauri Mahakama kama washtakiwa wana hatia au la.
Miriam Mrita, mke wa aliyekuwa mfanyabiashara wa madini mkoani Arusha, Erasto Msuya anakabiliwa na kesi moja ya mauaji ya wifi yake Aneth Msuya.
Aneth ambaye alikuwa mdogo wake bilionea Msuya aliuawa Mei 26, 2016 kwa kuchinjwa nyumbani kwake Kibada, Kigamboni, wilayani Temeke (wakati huo), jijini Dar es Salaam.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live