Mnamo tarehe 29/09/2022, Mahakama ya Wilaya Mbarali ilitoa hukumu katika shauri la Uhujumu Uchumi Na. 17/2022 dhidi ya George Kagomba, Ferdinand Manyele, Ponsiano Ngwando na Yasini Kabelege.
Ambapo washitakiwa wa 1-3 Walikuwa watumishi Halmashauri ya Wilaya Mbarali kwenye nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji, Mweka Hazina na Afisa Mtendaji wa Kata mtawalia na mshitakiwa wa 4 alikuwa Makamu Mwenyekiti - Kamati ya Ujenzi katika Shule ya Sekondari Rujewa.
Washitakiwa hao walishitakiwa kwa makosa 4 ya Ubadhilifu wa shs 11,765,000/=, Kughushi, Kutumia Nyaraka kwa Lengo la Kumdanfanya Mwajiri na Kuwasilisha Nyaraka za Uongo. Mahakama kwenye uamuzi wake imewatia hatiani Washtakiwa wote 4 kwa Makosa hayo na kila mmoja kuadhibiwa kulipa fine au kwenda Jela miezi 6. Pia wameamriwa.
kurejesha kiasi chote cha shs. 11,765,000/= walichofuja.