Mon, 6 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) imewafikisha Mahakamani watu 6 wa Mamlaka ya Maji Jijini Arusha (AUWSA) kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka, kula njama na kujipatia Tsh. Bilioni 5.3.
Walitenda makosa hayo kati ya Desemba 2017 na Oktoba 2018, ambapo walikula njama kupitia Mradi wa Maji wa Kanda bila kufuata taratibu za manunuzi.
Waliokamatwa ni pamoja na aliyekuwa Mkurugenzi wa AUWSA, Mhandisi Ruth Koya na Mkurugenzi wa Kampuni ya Kiure Engineering, Omari Kiure.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live