Tue, 14 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoani Arusha limewakamata watuhumiwa 188 kwa tuhuma za makosa mbalimbali ikiwemo ya wizi na usafirishaji wa dawa za kulevya.
Akitoa taarifa hiyo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi wa Polisi, ACP Salvas Makweli leo Jumanne Novemba 14, 2023 amesema jeshi hilo lilifanya operesheni maalum kuanzia Oktoba 13 hadi Novemba 13 mwaka huu kwa lengo la kuwakamata watuhumiwa wanaojihusisha na matukio hayo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live