Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu watatu wahukumiwa kifungo cha maisha jela mkoani Kagera (video)

1024 SHERIA TZW

Thu, 4 Jan 2018 Chanzo: millardayo.com

January 3, 2018 Mahakama ya Wilaya Bukoba imewahukumu kifungo cha maisha washtakiwa watatu kwa makosa mawili, kosa la kwanza likiwa ni kula njama ya kutenda kosa na kosa la pili kuchoma kanisa la EAGT lililokuwa kata ya Kibeta katika Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Wilaya ya Bukoba CHARLES OWISSO amesema kuwa washtakiwa hao ambao ni ALIYU DAUDA, NGESERA JOSEPH na RASHIDI ATHUMANI walitenda makosa hayo September 22, 2015.

Wakiongea nje ya Mahakama Mawakili wa Serikali Haruna Shomali na Emmanuel Kaigi wamesema kuwa washtakiwa hao wamepata adhabu inayowastahili huku wakiongeza kuwa washtakiwa hao walikuwa wanatumikia adhabu nyingine ya kifungo cha maisha baada ya kutenda kosa la kutoa watu koromeo maeneno mbalimbali ya Mkoani Kagera

VIDEO: KESI YA UHUJUMU UCHUMI INAYOMKABILI KALUGENDO NA MWENZAKE ITASIKILIZWA MAHAKAMA YA MAFISADI?

Chanzo: millardayo.com