Sun, 12 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu wasiofahamika wamevamia na kufanya uharibifu wa mali katika nyumba anayoishi Mbunge na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole Jijini Dodoma.
Pole pole amesema watu hao wamevamia na kuiba Televisheni na kupekua katika sehemu kubwa ya nyumba yake wakati yeye akiwa safarini Mkoani Manyara.
Kwa sasa Polepole amekwenda kutoa taarifa kituo cha Polisi kwa ajili ya hatua zaidi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live