Tue, 24 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Watu 35 wamekamatwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma ya kukutwa na KG 51.16 za dawa za kulevya Mkoani Dodoma kati ya mwezi November 2022 hadi January 2023.
RPC wa Dodoma, Kamishna Msaidizi wa Polisi Martin Otieno amesema miongoni mwa waliokamatwa ni Wauzaji na Watumiaji wa dawa hizo.
"Jumla ya Watuhumiwa 35 ambao ni Wauzaji na Watumiaji wa dawa za kulevya na kiasi kilichokamatwa ni takribani kilogramu 51.16"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live