Jeshi la polisi Mkoa wa Rukwa limewakamata watu 173 wanaojihusisha na vitendo vya kishirikina maarufu lama lambalamba ikiwa ni mwendelezo wa jitihada za kukomesha vitendo hivyo mkoani humo
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Rukwa ACP - Theopista Mallya anasema watuhumiwa 95 walikamatwa katika Wilaya ya Nkasi na watuhumiwa 78 katika Wilaya ya Kalambo
Inaelezwa kuwa watu hao wamekuwa wakichochea vitendo hivyo vya kishirikina na kusababisha uvunjifu wa amani katika mkoa huo ambapo tayari watuhumiwa hao wamefikishwa mahakamani.
Katika hatua nyingine jeshi la polisi limefanikiwa kumkamata mtu mmoja akiwa na silaha aina ya Gobole kinyume na sheria, mwingine na Nyara za serikali ambazo ni Ngozi ya Paka Pori na mtuhumiwa mwingine amekamatwa akiwa na vitu ambavyo vinazaniwa kuwa vya wizi zikiwemo TV 3 na Redio Moja.