Watu 17 wamekamatwa kwa tuhuma za kutaka kuwafanyia Mitihani Wanafunzi wa Chuo Kikuu Huria (OUT) katika Vituo vya Ilala (Watuhumiwa 13) na Kinondoni (Watuhumiwa 4)
Makamu Mkuu wa OUT, Prof. Elifas Bisanda ameliomba Jeshi la Polisi kuwafikisha Mahakamani haraka Watuhumiwa ambao asilimia kubwa ni Watu wa Nje na hawana uhusiano na Chuo, akidai walitumia Vitambulisho vya wale waliotaka kufanyiwa Mitihani na wengine walighushi Vitambulisho jambo ambalo ni kosa la Jinai
Ameongeza “Hatujui wamelipwa kiasi gani, matukio yalianza kuripotiwa Juni 18, 2024, tuliwakamata kwa msaada wa Wasimamizi wetu na Maafisa wa Usalama wa Taifa. Tupo tayari kutoa ushirikiano kwa Polisi, vielelezo vyote tunavyo. Sitaridhika kusikia wanaendelea na upelelezi wakati ushahidi wote upo na nitaifikisha taarifa hii kwa IGP na Ofisi ya Rais.”