Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watu 14 wakamatwa kwa kuvamia kituo cha polisi

Fadhsdthfy.jpeg Watu 14 wakamatwa kwa kuvamia kituo cha polisi

Fri, 3 Dec 2021 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Watu kumi na nne wakazi wa mji wa Gairo wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa Morogoro kwa tuhuma za Kuvamia kituo Cha polisi Gairo wakishinikiza polisi kuwaachia watuhumiwa watatu wanaodaiwa kuhusika na mauaji ya Bodaboda yaliyotokea hivi karibuni wilayani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari kamanda wa polisi mkoa Morogoro Fortunatus Musilimu amesema watu hao ambao wengi Ni madereva Bodaboda walianza Kuvamia nyumba za watuhumiwa wa mauji na kuanza kuzibomoa Kisha kuhamia kituo Cha polisi Cha Gairo na kuanza kufanya fujo.

Kamamda Musilimu amesema baada ya kutokea Hali hiyo wakawakamata watu kumi na nne ambao wanadaiwa kuhusika kufanya fujo katika kituo hicho Cha polisi na uharibufu wa nyumba za Watuhumiwa wa mauaji

Chanzo: www.tanzaniaweb.live