Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Watatu kortini kwa kukutwa na vipande vya meno ya tembo

Wed, 22 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es  Salaam.  Watu watatu wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Jumanne Mei 21, 2019 wakikabiliwa na mashtaka mawili,  likiwemo la kukutwa na vipande vya meno ya tembo yenye thamani ya Sh69milioni.

Wakili wa Serikali, Candid Nasua amewataja  washtakiwa hao kuwa ni Godlisten Mtume (31), Frank Lucas(24) na Mhando Shomary (37).

Akiwasomea hati ya mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde, Nasua amedai washtakiwa hao wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 40/2019.

Amedai katika shtaka la kwanza, washtakiwa kwa pamoja wanadaiwa Mei 7, 2019 Mbezi Luis jijini Dar es Salaam walikutwa na vipande vinne vya meno ya tembo vyenye thamani ya dola 30,000 za Marekani sawa na Sh69milioni  mali ya Serikali ya Tanzania.

Nasua amedai washtakiwa hao walikutwa na vipande hivyo bila kuwa na  kibali kutoka kwa mkurugenzi wa wanyamapori nchini.

Katika shtaka la  pili, siku na eneo hilo, washtakiwa walitakatisha Sh69milioni, fedha zilizotokana na malipo ya uwindaji.

Pia Soma

Baada ya washtakiwa kusomewa mashtaka hayo, hakimu Kasonde amesema hawatakiwi kujibu chochote mahakamani hapo kutokana na mashtaka yanayowakabili kutokuwa na dhamana.

Nasua amedai upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kuomba  tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa na Hakimu Kasonde kuahirisha shauri hiyo hadi Juni 4, 2019.

Chanzo: mwananchi.co.tz