Dar es Salaam. Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewafutia mashtaka na kuwaachia huru washtakiwa watano waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi kwa kujiunganishia isivyo halali bomba la mafuta, mali ya Mamlaka ya Bandari Tanzania ( TPA).
Soma zaidi: Wakili akwamisha kesi ya bomba la mafuta
Uamuzi huo umetolewa leo Jumatatu Septemba 23, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania (DPP) kuieleza Mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na kesi hiyo.
Walioachiwa huru ni Audai Ismail (43) Chibony Emmanuel, Roman Abdon, Amina Shaban na Zubery Ally.
Endelea kufuatililia Mwananchi kwa taarifa zaidi
SOMA ZAIDI: Washtakiwa kesi ya bomba la mafuta waendelea kusota rumande