Watu wasiojulikana wamevunja ofisi ya mhasibu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Nronga, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro na kuiba fedha zaidi ya Sh3 milioni za sadaka na Kompyuta mpakato yenye thamani ya Sh780, 000.
Watu wasiojulikana wamevunja ofisi ya mhasibu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Nronga, Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro na kuiba fedha zaidi ya Sh3 milioni za sadaka na Kompyuta mpakato yenye thamani ya Sh780, 000. Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo Januari 8, 2024, na uchunguzi wa tukio hilo bado unaendelea.