Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wasiojulikana waua mwanamke Moshi

Auawa Pc Marehemu, Elice Matafu

Tue, 31 Aug 2021 Chanzo: Mwananchi

Elice Matafu, Mkazi wa Kijiji cha Mrimbo Uuwo, Kata ya Mwika Kaskazini, Wilaya ya Moshi ameuawa kwa kukatwa shingo na watu wasiojulikana nyumbani kwake, usiku wa saa 2.

Kamanda wa Polisi Mkoani Kilimanjaro, Simon Maigwa amethibitisha kuuawa kwa mwanamke huyo na amesema mauaji hayo yanaviashiria vya visasi ambapo tayari anashikiliwa kijana mmoja kwa mahojiano zaidi.

"Ni kweli huyu mwanamke ameuliwa nyumbani kwake usiku kwa kukatwa shingo na inaonekana kuna viashiria vya visasi, tayari tunamshikilia kijana mmoja kwa mahojiano zaidi,"amesema Kamanda Maigwa.

Kamanda Maigwa amesema wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini hasa chanzo cha mauaji hayo.

Chanzo: Mwananchi