Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Washukiwa wawili waliotoroka mikononi mwa polisi wanaswa tena

1b03301c2cdff851 Washukiwa wawili waliotoroka mikononi mwa polisi wanaswa tena

Wed, 17 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

< Washukiwa wawili ambao walikuwa wamefanikiwa kuwashinda maarifa maafisa wa polisi wa kituo kimoja kilichoko chini ya ulinzi mkali na kuhepa.Wawili hao wanasemekana kupanga njama ya kutoroka kizuizini, mpango walioutekeleza mnamo Alhamisi,11Novemba. Washukiwa hao ni Elvis Odhiambo na Mohammed Aden Hussein, wanakabiliwa na kesi ya wizi na kimabavu kutoka Kituo cha Polisi cha Kapsoya mjini Eldoret na kusababshwa Polisi kuanzisha msako uliodumu kwa takrim wiki nzima wamewakamata.

Wawili hao walinaswa baada ya kikosi cha maafisa wa polisi kutoka kaunti za Uasin Gishu na Kisumu kutumwa kuwasaka washukiwa hao.

Walikamatwa katika eneo la Manyatta mjini Kisumu, maafisa kutoka vituo vya polisi vya Kondele na Kapsoya.

"Mohammed Aden Hussein wa miaka 18 na Elvis Odhiambo miaka 17 walikuwa wanakabiliwa na mashtaka ya wizi katika Mahakama ya Eldoret," ripoti hiyo ilisema.

"Washukiwa hao wawili wanazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Kondele ambapo wanasubiri kusafirishwa hadi Kapsoya."

Haya yanajiri huku polisi wakiimarisha msako wa kuwatafuta wafungwa wengine watatu wa ugaidi waliotoroka katika gereza kuu la Kamiti mnamo Jumatatu usiku, Novemba 15.

Ripoti za awali zilifichua kuwa watatu hao walitoboa tundu kwenye ukuta kabla ya kutoroka.

Wapelelezi pia waliripoti kuwa watatu hao ambao wametajwa kuwa hatari, walitumia wembe kukata blanketi walizotumia kama kamba ya kuwasaida kuteremka kwenye kuta katika refu za gereza la Kamiti.

Wapelelezi wakiongozwa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Jinai (DCI) George Kinoti wanajaribu kubaini jinsi wafungwa hao wa kigaidi walivyofankiwa kuhepa kutoka gereza hilo ambalo lipo chini ya ulinzi mkali.

Watoro hao Joseph Juma Odhiambo almaarufu Yusuf, Musharaf Abdalla Akhulunga almaarufu Zarkawi, na Mohamed Ali Abikar - ambao walikuwa wametiwa mbaroni kutokana na shughuli za kigaid

Uasin Gishu: Washukiwa wa Wizi wa Kimabavu Wahepa Seli Baada ya Kuwazubaisha Polisi

"Hatutaenda tu kama uchunguzi utatuelekeza, lakini tutachukua hatua kuhakikisha uzembe wa aina hii hautokei tena kwa sababu unahatarisha maisha yetu sote. Kwa hakika, kuna kiwango fulani cha kutowajibika tunachopaswa kushughulikia katika kesi hii mahususi,” Waziri wa Usalama wa Ndani Fred Matiang'i alisema katika taarifa iliyotolewa Jumanne, Novemba 16.

Maafisa watatu wa magereza wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke