Mon, 27 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro limeshtukia mbinu zinazotumiwa na baadhi ya madereva wa mabasi madogo aina ya Costa kusafirisha abiria bila ya kuwa na kibali kwa kivuli cha kubeba marehemu.
Jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro limeshtukia mbinu zinazotumiwa na baadhi ya madereva wa mabasi madogo aina ya Costa kusafirisha abiria bila ya kuwa na kibali kwa kivuli cha kubeba marehemu. Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi wa Polisi Saiomon Maigwa amesema kwa sasa oparesheni kali inaendelea ili kuwabaini wahusika wote na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live