Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wapenzi mbaroni kwa kumuua bibi mwenye miaka 100

Wapenzi Pic Data Wapenzi mbaroni kwa kumuua bibi mwenye miaka 100

Wed, 24 Aug 2022 Chanzo: Mwananchi

Wapenzi wawili wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma za kumuua bibi kizee wa miaka 100 kwa kumpiga na kitu kizito kichwani wakati wakigombea ardhi.

Bibi huyo, Felister Silayo, mkazi wa Kijiji cha Kirongo juu, Kata ya Kirongo Samanga, Wilaya ya Rombo alifikwa na umauti Agosti 13 akiwa nyumbani kwake baada ya kuvamiwa na watu hao na kupigwa na kitu kizito kichwani wakati akiingiza ndani majani ya mbuzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alisema juzi kuwa wapenzi hao walikamatwa juzi na sasa wanaandaa jalada kwa ajili ya kupeleka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

“Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro tunawashikilia watu wawili ambao ni wapenzi kwa tuhuma za mauaji ya bibi kizee. Baada ya tukio tulifanikiwa kumkamata mwanamke na kwa bahati mbaya mpenzi wake alitoroka, lakini jana tumemkamata na wote wawili tunao,” alisema.

Kamanda Maigwa alisema chanzo cha mauaji hayo ni mgogoro wa ardhi uliokuwepo muda mrefu tangu mwaka 1990 kati ya bibi huyo na mtoto huyo a kike.

Kutokna na tukio hilo, kamanda Maigwa aliwasihi wananchi kupata hati miliki ya ardhi, ili kuepuka migogoro ya ardhi inayosababisha uvunjifu wa amani na mauji kama hayo.

Bibi huyo alizikwa Agosti 20 nyumbani kwake kijiji cha Kirongo juu, kata ya Kirongo Samanga.

Awali, ndugu wa bibi huyo, Plasidi Constantine (60) alidai bibi huyo alikuwa na watoto wawili--- mmoja wa wa kiume na mwingine wa kike na kila mmoja alimpa shamba lake, baada ya mgawanyo wa mashamba mtoto huyo wa kike aligoma kuondoka nyumbani akitaka kuchukua maeneo yote, jambo ambalo lilileta mgogoro.

Aliekeza kuwa hali hiyo ilisababisha mtoto huyo wa kiume kutoroka nyumbani.

“Cha kushangaza huyu mtoto wa kike baada ya kupewa eneo laake hakutaka kuondoka hapa nyumbani kwa huyu bibi akawa anang’ang’ania kukaa.

Alitaka kuchukua maeneo yote mawili...mwisho wa siku ndio hivyo huyu bibi ameuawa. Kwa kweli tunasikitika,” alisema.

Chanzo: Mwananchi