Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waomba kumaliza kesi nje ya mahakama

101566 Pic+katani Waomba kumaliza kesi nje ya mahakama

Wed, 8 Apr 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Tanga. Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga imetaarifiwa juu ya nia ya washtakiwa wa kesi ya uhujumu uchumi ya Katani Limited kuomba kuiondoa kesi hiyo mahakamani na kujadiliana nje ya mahakama.

Mbele ya Hakimu Mkuu Mkazi, Ruth Mkisi kesi hiyo ilipoletwa kwa ajili ya kutajwa kesi wakili wa washtakiwa hao wawili Warehema Kibaha aliiambia mahakama hiyo kwamba Ofisi ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali imepelekewa barua ya maombi hayo, lakini bado haijajibu.

Baada ya kusikilizwa maombi hayo ya washtakiwa, Hakimu Mkisi aliahirisha shauri hilo hadi Mei 05, 2020 litakapotajwa tena na washtakiwa wote wawili wamerudishwa rumande.

Katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi ya mwaka 2019 iliyowahusu washtakiwa watatu, Salum Shamte, Juma Shamte na Fatuma Diwani, mshtakiwa wa kwanza alifariki dunia wiki iliyopita na hivyo kubaki washtakiwa wawili.

Chanzo: mwananchi.co.tz