Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wananchi wataka DJ Brownskin akamatwe kwa kumrekodi mkewe akijiua

Brownskin Df.jpeg Wananchi wataka DJ Brownskin akamatwe kwa kumrekodi mkewe akijiua

Sun, 2 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Wakenya wengi kwenye mitandao ya kijamii wamebaki vinywa wazi baada ya video kuvuja ikionesha jinsi DJ BROWNSKIN alimrekodi mkewe akijitoa uhai.

Marehemu Sharon Njeri Mwangi anasikika akisema kuwa anataka kujitoa uhai ambapo anachanganya dawa na sumu ndani ya kikombe kisha kunywa kwa haraka huku mumewe akimrekodi.

Baada ya kubugia sumu anaketi chini akiwa hoi bin taabani huku akimwita mwanae kusudi amuage kwaheri.

"Papa! Papa! Mimi nakufa." Anasema Njeri huku nguvu zikianza kumuishia.

Dakika chache baadae anaanguka sakafuni akilia kwa uchungu na hapo sasa ndipo mumewe anamuagiza mfanayakazi wa nyumbani kumletea Njeri maziwa, lakini juhudi hizo hazikufua dafu kwani Njeri alifariki dunia.

Yote haya yalitendeka mbele ya mtoto wao wa kiume anayesikika akimwita mamake anywe maziwa.

Ikumbukwe aliaga dunia mwaka uliopita lakini video imevuja Leo Jumapili , Aprili 2, 2023.

Wakenya sasa wametoa rai kwa idara ya upelelezi wa jinai DCI kumkamata DJ Brownskin wakidai kuwa alihusika kwa namna moja ama nyingine.

Endapo atakamatwa basi huenda Brownskin akawa na kesi ya kujibu kwa mujibu wa Sheria za Kenya kama ifuatavyo:

• Kusaidia mtu kujitoa uhai.

• mauaji ya kutokukusudia (involuntary manslaughter)

• 'Child torture' kwani kisa chote hicho kilinakiliwa mbele ya mtoto.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live