Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wanaigeria waandika barua kwa DPP, wakiri makosa

81607 Pic+mahakamani Wanaigeria waandika barua kwa DPP, wakiri makosa

Fri, 25 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Raia watatu wa Nigeria  akiwemo mchungaji wameandika barua kwa mkurugenzi wa mashtaka nchini Tanzania (DPP) kukiri kosa la uhujumu uchumi linalowakabili.

Washtakiwa hao, Henry Ozoemana Ogwuanyi (mchungaji), Onyebuchi Ogbu na Lucy Oding

wanakabiliwa na kesi ya kukutwa na kilo 15.8 za dawa za kulevya aina ya Heroin.

Wakili wa Serikali, Elia Athanas ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Alhamisi Oktoba 24, 2019 kuwa washtakiwa hao wameandika barua  kwa DPP kwa ajili ya kuomba msamaha na kukiri makosa yanayowakabili.

"Washtakiwa wameandika barua ya kukiri makosa yao lakini DPP bado hajajibu barua hiyo, naiomba mahakama ipange tarehe nyingine,” amedai Athanas.

Baada ya maelezo hayo wakili wa utetezi, Hassan Kiangio amedai suala la kuandika barua kwa washtakiwa hao isiwe kikwazo cha kutoendelea na kesi hiyo, kuuomba  upande wa mashtaka kukamilisha upelelezi ili shauri hilo liende mbele.

Habari zinazohusiana na hii

Advertisement
Hakimu Shaidi ameahirisha shauri hilo hadi Novemba 6, 2019 itakapotajwa.

Katika kesi ya msingi inadaiwa Aprili 21, 2019  eneo la Msimbazi wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam washtakiwa walikutwa na dawa za kulevya aina ya Heroin kilo 15.8.

Chanzo: mwananchi.co.tz