Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waliojifanya askari wajeruhi kwa panga, wapora simu na Sh45, 000

Picha Waliojifanya Data Waliojifanya askari wajeruhi kwa panga, wapora simu na Sh45, 000

Tue, 18 Jul 2023 Chanzo: mwanachidigital

Watu watatu wa familia moja wakazi wa Kijiji cha Isima Wilaya ya Geita wamejeruhiwa kwa kukatwa panga na watu waliojifanya kuwa askari ambao pia wamepora mahindi, simu ya kiganjani na fedha taslimu Sh45, 000.

Taarifa zilipatikana kutoka kijijini hapo zinaeleza kuwa kabla ya kutenda uhalifu huo, watuhimiwa hao wanadaiwa kufika kwenye familia na kujitambulisha kuwa askari polisi waliokuwa wakifanya msako kwenye nyumba hiyo.

Akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu leo Julai 17, 2023, Mkuu wa Wilaya ya Geita, Cornel Maghembe amesema majeruhi wa tukio hilo tayari wamefikishwa Hospitali ya Halmashauri ya Mji Geita kwa matibabu.

“Jeshi la polisi linaendelea na msako dhidi ya waliohusika katika uhalifu huo,’’ amesema DC Maghembe

Muuguzi katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji Geita, Emanuel Gidion amethibitisha kupokelewa kwa majeruhi watatu, wanaume wawili na mwanamke waliofikishwa hositalini hapo alasiri ya Julai 16,2023.

Tukio lilivyotokea

Akizungumzia tukio hilo, Maneno Stephen, mmoja wa majeruhi aliyelazwa hospitalini kwa matibabu amesema alikutana na wawili kati ya watuhumiwa ambao walikuwa wamepanda pikipiki amboa walijitambulisha kwake kuwa wao ni askari polisi huku wakimwamuru kukaa chini.

“Nikiwa bado najishauri huku nikijiuliza kosa langu, watu wale walinipiga ngumi eneo la tumboni na ghafla wakatoa panga wakitaka kunikata shingoni. Nilijiviringisha kukwepa panga na kufanikiwa kunyanyuka na kutimua mbio lakini wakafanikiwa kunishika na kuanza kunikata kwa panga sehemu mbalimbali za mwili,” amesema Stephen

Amesema watu hao pia walikuwa na ubao uliochongwa mfano wa bunduki huku akiliomba Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kuwabaini wahusika ili wachukuliwe hatua za kisheria.

Joram Hamis, mmoja wa ndugu wa majeruhi hao amesema siku ya tukio, watu wawili wasioahamika walifika nyumbani kwa shemeji yake na kumfunga kamba, wakamfungia ndani ya chumba kabla kuanza kumshambulia kwa kumkata panga mume wake alipojaribu kumtetea mke wake.

Chanzo: mwanachidigital