Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Waliogoma kupeleka watoto shule wakidai MUNGU anakataza wafikishwa Mahakamani (+video)

Maxresdefault 42 660x400 Waliogoma kupeleka watoto shule wakidai MUNGU anakataza wafikishwa Mahakamani (+video)

Thu, 11 Feb 2021 Chanzo: millardayo.com

Mchungaji Marchades Buberwa na Mke wake Wakazi wa Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera walioripotiwa hivi karibuni kugoma kupeleka Watoto Shule kwa madai kuwa Mungu wanaemuabudu amewakataza kufanya hivyo, wamefikishwa Mahakamani Bukoba.

Wamesomewa mashtaka nane likiwemo la kushindwa kutimiza wajibu wao kama Wazazi kwa kutopeleka Watoto wao shule kinyume cha sheria ya elimu na sheria ya Mtoto ya mwaka 2009.

Washtakiwa wote wawili wamekana mashtaka hayo na kuachiwa kwa dhamana huku kesi hiyo ikiahirishwa hadi February 25 mwaka huu.